Kuhusu maboresho ya nywele Joketi alisema "Tulipotoa bidhaa za mwanzo, honestly kuna watu walisema kuna vitu ambavyo walipenda viboreshwe zaidi na sasa hivi kweli vimeboreshwa. Packaging imeboreshwa, sasa hivi tumeweka kifungo.” "Ni bidhaa ya nyumbani, ni bidhaa inayotengenezwa na mwanamke, kwa hiyo naelewa wanawake wanahitaji nini. Ni bidhaa ambayo bei yake sio kubwa lakini quality yake ni nzuri, mtu anaweza kuvaa kwa mwezi na isimuwashe kichwani. Kwa hiyo ni kitu ambacho tumekipackage vizuri, vilevile kina muonekano mzuri, rangi tumechagua nzuri. Kwa hiyo zinashindana vizuri tu na bidhaa za nchi nyingine,” ameongeza.
Joketi alimaliza kwa kusema "“Nimelenga hasa East na Central Africa, kwa sababu nimeshaanza kupata order kutoka Burundi, Kenya..yeah kwa hiyo ni East na Central Africa. Kuhusu mikoani, sasa hivi mimi nadeal kwanza na Agents, agents wangu wengi wako Kariakoo na ndio wanaopeleka mikoani. Sijaanza kupeleka moja kwa moja mikoani, hiyo ndio njia ninayoitumia kupeleka mikoani.”
No comments:
Post a Comment